Kiungo wa klabu bingwa nchini Hispania, Andres Iniesta amepingana na vyombo vya habari vya nchini England, vinavyoendelea kulikuza sakata la uhamisho wa beki wa klabu ya Real Madrid, Sergio Ramos. Iniesta amesema suala la kuondoka na Ramos nchini Hispania na kujiunga na klabu ya Man Utd kwake halipo na katu hawezi kulikubali kutokana na kuamini kwamba Los Blancos hawawezi kumuachia beki huyo. Amesema, Sergio Ramos ni beki anayetumainiwa kwa kiasi kikubwa katika klabu hiyo ya mjini Madrid na endapo atakubaliwa kuondoka, pengo lake haliwezi kuzibika kirahisi. Hata hivyo Iniesta amesema Man Utd ni klabu kubwa kama ilivyo Real Madrid, na inaweza kufanya lolote katika mipango ya usajili ya beki huyo mwenye umri wa miaka 29, lakini bado akaendelea kusisitiza kizingiti cha kubaki kwa Ramos kitaendelea kuwa viongozi wake. Ramos amekua akihusishwa na mipango ya kutaka kuhamia Old Trafford baada ya kuibuka mzozo kati yake na viongozi wa klabu ya Real Madrid unaohusu thamani ya mkataba wake mpya ambao bado hajausaini FOLLOW INSTAGRAM@sosteneslekule
[via LEKULE]
Follow us @automobileheat – lists / @sectorheat